JIFUNZE JINSI YA KUANDIKA MISWADA YA FILAMU [SCRIPT]

Tanzania ina muda mrefu kiasi katika tasnia ya filamu maarufu kama BONGO MOVIE na hadi kufikia sasa ina mafanikio,lakini sio mafanikio ya kutosha kulinganisha na nchi zingine zinazofanya tasnia hii,mfano,Nigeria,India,Afrika ya kusini na Kenya n.k. Zipo sababu nyingi za kwanini tasnia hii ya filamu ni changa bado na isiyolipa kulinganisha nchi zingine na kwingine. Hizi ni baadhi ya sababu  
                                                                                                                                                                     1. Script zilizokosa ubunifu  2  Technolojia duni  3 kukosa waigizaji wenye vipaji na ubunifu  4. Elimu ndogo kwa waongoza filamu [directors]  na wazalishaji [ producers] 5. Umaskini wa kifedha na budget isiyo na mpangilio   ,6. Wizi wa kazi za wasaniina 7 kukosa suport kutoka kwenye vyombo vinavyosimamia utamaduni na michezo [serikari]  7. Utandawazi.hizo ni baadhi ya sababu zinazofanya tasnia ya filamu tanzania BONGO MOVIE  kukosa ubora Script/muswada wa filamu,ni moyo wa tasnia hii. Nadiriki kuita moyo maana hii ndiyo inayohamasisha filamu ichezwe au la!, na baada ya maamuzi ndiyo inayotoa muongozi wa sauti,picha na mazungumzo kama itavyoonekana kwenye tv. Script ni angalabu kuwa ya mtu mmoja,mara nyingi itapokea mabadiliko kulingana na tafsiri za wadau mbalimbali,maoni yao na mitizamo wao. Mfano director au waigizaji huweza kushauri mabadiliko. Kuandika muswada mzuri ni lazima upangilie sauti,picha,mazungumzo na matendo yote kwa ujumla kwa namna ambavyo unachokiwaza kitafsiriwe sawia na kuonekana kupitia tv sawa na mawazoni,ili kutimiza hili,mwandishi anatakiwa apate uzoefu kwa kupitia miswada ya filamu anazopenda na zilizotamba kisha azipitie kwa kusoma kwa hisia namna uhusika unavyovikwa kwa waigizaji,mpangilio wa uandishi wa mazungumzo na matendo
Kama tayari una idea ya stori,basi ainisha kwanza sehemu nzuri za kufanyia hiyo idea,mahusiano ya characters,tabia na wasifu wao. Lazima pia ujue ni idea ipi imebeba story yako nzima na namna hao characters watashirikiana kuikamilisha idea hiyo. Idea nzuri sio lazima iwe ile ambayo haijawahi kusikika,bali ni ile ambayo inasisimua na inatoa nafasi ya matukio mengi kufanyika ili kuikamilisha,mfano,ninataka kuandika kuhusu pete ya ajabu,kama part muhmu ya script yangu,basi humu ndani nitaweka visa vya kimapenzi vyenye uhalifu,uchawi na ucheshi. Lakini vyote hivi viwe vinatukia kwasabubu ya pete ya ajabu. Mfano mbaya wa idea ya stori kwa wakati huu ni,story ambayo part yake muhmu ni usaliti wa mapenzi tu,eti baba anatembea na mfanyakazi wa ndani yaani ndio kisa tu!.
Kuchagua idea ya story ya kuandikia script inategemea vitu kadhaa,kwanza bajeti ya yule unaye mwandikia na uwezo wa kiteknolojia,huwezi ukaandika kuhusu kuzama kwa mv Bukoba kwa mfano,maana imagination hazilipiwi hivyo unaweza kuandika chochote,lakini haitatendewa haki na yule unamwandikia.
Kingine usichague idea ambazo haupo mahiri na huru kwazo,mpaka pale utapo kuwa tayari kujifunza na kufanya risechi juu ya mambo yanayohusu idea hiyo,mfano kuhusu upelelezi! Kuandika movie ya kipelelezi lazima uwe na taarifa muhimu na halisia juu ya mambo ya kipelelezi na uwe na uwezo wa kuwa mbunifu kiupelelezi au upate mtu mwenye uwezo huo ahusike katika kuchangia ujuzi.
Idea sio lazima iwe na uhalisia,wa asilimia mia,japo inategemea ni aina gani ya uandishi unafanya,kama ni based on true sawa,lakini komedi na zingine sio lazima. Hapa naongelea pia katika mazungumzo ya kwenye script,dialogues ni kawaida zitofautiane na kua za kibunifu tofauti na zile za maisha halisi,maana dialogue za kwenye script zinakua na uhai zenye speed ya kutimiza lengo fulani wakati za maishani hazina haraka,kwa kuwa muda haubani wala budget,wala hazikaririwi,hivi ni muhimu mazungumzo yawe ya ubunifu wa kusisimua,na fupi lakini yenye lengo mahususi kuhusiana na story.
Lingine usiwe na haraka ya uandishi,jipe muda wa kufikiria na kuyapangilia mawazo katika mtiririko unaoeleweka. Kutimiza hili gawa story yako katika vipengele vitatu, 1. Utangulizi-hapa unawatambulisha wahusika na mahusiano yao,wasifu,pia chanzo cha kisa. 2. Mgogoro-hapa kisa kimetokea na namna kinavyoathiri wahusika. 3. Hitimisho-kisa kile kimeshaleta madhara,namna ya utatuzi umefanyika,wabaya wanalipwa,wazuri wanafaidika zaidi,mwisho
Baada ya kufanya hayo yote,basi ni wakati muafaka wa kuandikika katika mpangilio unaokubalika na kueleweka,kumbuka ili kubuni na kuandika kitu kizuri,’MAZINGIRA’ yana influence kubwa kwenye fikra. Kaa mahali panapokufanya emotional na kukupa amani moyoni (mfano mimi napenda kuandika sehemu yenye upepo na juu kidogo,hii hunifanya kuwa na connection nzuri na hisia hasa pale ninapoandika kuhusu romance na maumivu),wengine hupenda kuandika kwenye chumba cha rangi flani,mfano,unaandika kuhusu maovu ukikaa chumba chenye mwanga hafifu kama nyeusi au nyekundu,au kusikiliza nyimbo za miondoko ya hip hop basi utakua inspired zaidi kupata idea za vurugu,huwezi kuandika romance ukiwa baa au mahali pa vurugu,wengine hupendelea kinywaji,mi nakubaliana nao lakini iwe kwa kiwango kidogo mno. Zipo software za bure na za kununua zitazoweza kukusaidia kufanya mpangilio automaticaly,mfano Montage,celtx,final draft n.k

TAFADHALI TUPE MAONI YAKO HAPA

Powered by Blogger.